Monday, October 4, 2010


Juzi jumanne nilipokea ujumbe kwenye simu yangu ya mkononi iliyosomeka KUNA TUKIO LA AINA YAKE,KUNA MDADA ANAWAKA MOTO BILA SABABU lakini maumivu hasikii tena kila anapokuwa unawaka hata akija kwako kukutembelea moto huwaka..Huku mburahati kwa jongo.

Hapo nyumbani inabidi ndugu wakae na ndugu yao maana moto huo unawaka akiwa peke yake bila watu,kukiwa na watu hauwaki.

Ndugu wakiwa katika hali ya simanzi kama kuna msiba kwa hicho kilichomkuta ndugu yao.

Ndugu wengi wamekusanyika hapo nyumbani kama kuna msiba vile,ili kukaa na ndugu yao kumfariji na kuhakikisha anakuwa sawa.

Alikuwa amekaa kwenye kochi kochi likaanza kuwaka moto,na lazima moto ukiwaka awe peke yake akija mtu mwingine unazima unabaki moshi.

Hili godoro liliungua wakati yeye amelala kitandani,likashika moto

Kaka wa mhanga wa tukio hilo akionyesha godoro lingine lililoungua kimaajabu.

Vitenge,nguo alizopewa na ndugu kuvaa pia ziliwaka kwa nyakati tofauti kwa siku unaweza kuwaka hata mara sita.

Nguo zilizoungua na zinaungua akiwepo yeye eneo hilo

Nguo mbalimbali zilizo ungua kwa nyakati tofauti....



Dada mwenyewe ndio huyu anaeonekana kidogo kwenye picha maana hakutaka kupigwa picha.Ni mjamzito hapo alipo ila hali ndio hiyo akiwa mahali hata kama ni kwako akikaa peke yake moto unawaka aidha kwenye nguo zake,kochi,kitanda,hata kama ni nguo iliyotundikwa inawaka moto.Mpaka sasa haijaeleweka ni kwa nini mashekhe wamemuombea dua toka juzi hiyohiyo ambapo alilala msikitini.
Wapo waliosema labda kachukua mume wa mtu kafanyiwa mchezo lakini alipoulizwa akasema huyo mwanaume mwenye mimba wamefunga ndoa na anavyojua kamkuta hana mwanamke labda awe kamdanganya.
Dada wa watu hana raha kabisa ndugu zake inabidi wakae nae kama kumetokea msiba maana ni kitu cha ajabu sana kilichompata ndugu yao maana kimeanza wiki hii hapa.



Mwisho kabisa moto huu haumuunguzi,wala hasikii maumivu ya aina yoyote zaidi ya hofu na wasiwasi wa kutokujua nini kipo nyuma ya huu moto.





WALEMAVU WAPANDA MLIMA KILIMANJARO:
Maaskari watatu wa zamani raia wa Marekani waliokatwa viungo vyao vya mwili wamepanda mlima Kilimanjaro, wakistahamili maporomoko na majeraha kufikia kilele cha mlima mrefu barani Afrika kila mmoja akiwa na mguu mmoja tu ambao ni imara.
Watu hao kutoka Vietnam, Afghanistan na Iraq, walikwea hadi kufikia juu ya mlima huo wenye urefu wa mita 5,891 uliopo nchini Tanzania.
Iliwachukua siku sita kufikia kileleni kwa nia ya kuonyesha kuwa ulemavu haumaanishi huna uwezo wa kufanya lolote.
Safari hiyo huchukua siku tano hadi sita, na ilibidi watu hao kusimama mara kwa mara ili kurekebisha miguu yao ya bandia, baada ya kuteleza sana.
Wakweaji hao wa mlima ni Dan Nevins, mwenye umri wa miaka 37, ambaye alipoteza miguu yake nchini Iraq, Neil Duncan, wa miaka 26, alipoteza miguu yote miwili katika shambulio la bomu lililotegwa barabarani Afghanistan mwaka 2005; na Kirk Bauer, mwenye miaka 62, aliyepoteza mguu mmoja huko Vietnam mwaka 1969.
Bw Bauer aliliambia shirika la habari la AP, " Ikiwa watu watatu waliokatwa viungo kutoka vita vitatu tofauti na kutoka vizazi tofauti na wana mguu mmoja tu wanaweza kupanda mlima Kilimanjaro, marafiki zetu wengine walemavu wanaweza kutoka na kupanda mlima au kuendesha basikeli au kuogelea, na wanaweza kuwa na maisha yenye afya njema."
Bw Nevis alipata jeraha katika kigutu ya moja ya miguu yake hiyo ya bandia na baada ya kufika kileleni aliondoshwa kwa kutumia machela.
Bw Bauer ni mkurugenzi mtendaji wa michezo ya walemavu wa Marekani, shirika lililopo mjini Wasington DC linaloshughulika na uzima wa afya na ushiriki wa michezo kwa walio na ulemavu.


FC Barcelona History - Historia ya klabu ya
balelona
                                  THE FC BARCELONA : MORE THAN A CLUB










On the 29th of November 1899, Joan Gamper founded the Football Club Barcelona ( Barça). Gamper chose the famous blue and claret as the team colours for they are the colours of the Swiss canton he came from. The myth was born: Kubala, Suárez, Cruyff, Maradona and Ronaldinho, among many others, have signed up for this Club. During the 20th century, "Barça" has become a Barcelona symbol, a symbol that represents the Catalan identity as a nation. That's why it is said that "Barça" is more than a Club.

THE MYTH IS BORN
In the Solé Gym office, on the 29th of November 1899, Gamper met Gualteri Wild, Lluís d'Ossó, Bartomeu Terrados, Otto Kunzle, Otto Maier, Enric Ducal, Pere Cabot, Carles Pujol, Josep Llobet, John Parsons and William Parsons. Eleven sportsmen gathered in order to found a football club. Gualteri Wild was appointed President. The 1st match contested was at the Bonanova Cycle Track and they played against a group of English expatriates who were living in Barcelona. The Englishmen won 1-0. On the 14th of March 1909, the Club inaugurated its 1st own ground at c/Indústria, with a capacity for 6,000 people. At that time, the Barcelona FC obtained their first victories: The Catalan Championships: 1909-1910, 1910-1911, 1912-1913, 1915-1916, 1918-1919 1919-1920, 1920-1921, 1921-1922 and the Spanish Championships: 1909-1910, 1911-1912, 1912-1913, 1919-1920 and 1921-1922.

LES CORTS STADIUM
The Les Corts ground (also known as "The Cathedral of Football") was inaugurated on the 20th of May 1922. That stadium had an initial capacity of 30,000 spectators but later doubled to 60,000. In 1924 the Club had already 12,207 members and a big number of supporters laid the foundations of the current social mass. During the season 1928-1929, Barça won brilliantly the 1st edition of the Spanish National League Title and ended, therefore, a period full of titles.
THE 30'S
Joan Gamper died on the 30th of July 1930. The decade which was about to start had a fatal beginning and the Club entered a period of decline: institutional crisis, many members left the Club, bad sports results and the Franco's supporters political pressure. The Civil War in 1936 had disastrous consequences for the FC Barcelona. Josep Suñol, President of the Club, was murdered by Franco's soldiers near Guadalajara. However, the Barça kept alive and in 1936 decided to go on tour around Mexico and the USA, fact that would help the Club financial problems. In March 1938 the fascists dropped a bomb on the FC Barcelona Social Club and cause serious damage. In 1939, the Franco's troops created many problems to the Club because it had already become a symbol to the Catalan people. The number of members also dropped to 3,486.
LA COPA LATINA (The Latin Cup)
During the 40's, Barça gradually recovered despite their internal difficulties. In June 1943, the scandalous game against Madrid in the Chamartín ground, saw the Barca players threatened by referee and police and Piñeyro, a fascist supporter, but honestly disgusted at the treatment his team had received, resigned from the presidency of the Club (which he had held since 1940). Better times were to come. Barça won the National League Titles 1944-45, 1947-48 and 1948-49 and the Latin Cup Title 1949, a competition which preceded the European Champions Cup Title, the FC Barcelona 1st international success. It was the time of César, Basora, Velasco, Curta, the Gonzalvo brothers, Seguer, Biosca o Ramallets. Barça celebrated their 50th anniversary reaching member numbers of 24,893.
KUBALA
Ladislao Kubala arrived in Barcelona in June 1950 and made the FC Barcelona become an unbeatable team thanks to their magic forward line: Basora, César, Kubala, Moreno and Manchón. Between 1951 and 1953, Barça won every competition on offer (Spanish Leagues 1951-52 and 1952-53 and Spanish Cups 1950-51, 1951-52 and 1952-53). From that golden period, it is important to emphasize the season 1951-52, in which they obtained the Five Cups: Spanish League, Spanish Cup, Latin Cup Eva Duarte and Martini Rossi trophies.

THE CAMP NOU, 1957

Kubala was too huge a figure for Les Corts and soon Francesc Miró-Sans promoted the building of the Camp Nou Stadium, which got inaugurated on the 24th September 1957. The new stadium had a capacity of 90,000.
Barça won the Spanish Leagues 1958-59 and 1959-60, and the Fairs' Cups 1957-1958 and 1959-60, coached by Helenio Herrera with such excellent players as Kocsis, Czibor, Evaristo, Kubala, Eulogio Martínez, Suárez, Villaverde, Olivella, Gensana, Segarra, Gràcia, Vergés and Tejada. The 60's were a period of crisis (they won the Spanish Cups 1963 and 1968 and the Fairs' Cup 1966, only). However, it was then that the sentence "more than a Club" was born. Barça was over the sports level: the Club and its colours became a way to defend the Catalan national identity.
CRUYFF
In 1973, the signing of Dutch Johan Cruyff put the finishing touches to a golden forward line of Rexach, Asensi, Cruyff, Sotil and Marcial, who led the league winning side of 1973-74. Coinciding with the Club's 75th anniversary, there were now 69,566 members, making it the most powerful sporting club in the World. Joan Miró did the commemorative poster of that event
JOSEP LLUÍS NUÑEZ
In 1978, Josep Lluís Núñez became President of the FC Barcelona. The Club then began a considerable period of social and financial expansion. The increase in member numbers reached the 100,000 and many supporter's clubs were founded. The FC Barcelona was becoming the sports most important entity in the world. Barça were also provided with emblematic sports facilities: the Camp Nou expansion (with a capacity of more than 100,000 spectators), the building of the Miniestadi, the Palau Blaugrana, and so on.
The Núñez era constitutes without any doubt the most brilliant sports moment in the Barça history: Basilea Cup Winner’s Cup, the Spanish League 1984-85, under Terry Venables, the Dream Team (1990-1994) under Johan Cruyff (four consecutive Spanish Leagues, the Cup Winners' Cup, the Spanish Cup and the Spanish Super Cup, and the European Champions Cup at the Wembley Stadium). Then came Bobby Robson, who won the Cup Winner's Cup, the Spanish Cup and the Spanish Super Cup in the 1996-97 season and Louis van Gaal's consecutive League Titles in 1997-98 and 1998-99, when the team won the double for the first time in 39 years.

TODAY'S BARÇA
The FC Barcelona is currently a sports entity which includes basketball, handball, hockey, athletism, ice-hockey, figure skating, indoor football, rugby, baseball, volleyball and women's football sections. The football team are the only side to have qualified for European competition every year since its inauguration in 1955. There are now a total of 105,706 members and 1,508 supporters clubs.
Mrehemu AMINA CHIFUPA
Mungu alailaze roho yake mahali pema paponi  AMIN........
lakini mtoto alikuwa na ......................Mhhhhhhhhhhhhh
  Mipango ya Mungu haikwepeki lakini tulitamani angekuwepo Amina atukumbushe enzi zake za leo tena kipindi hicho ikianza saa tatu asubuhi mpaka saa sita mchana.Tunamkumbuka japo hayuko nasi bado anaendelea kuishi na sisi mioyoni mwetu kwa kumbukumbu nzuri alizotuachia.Nakumbuka siku za mwisho kabla mwenyezi hajamchukua alikuwa kila siku ananiomba nimpigie wimbo wa Lady Jaydee siku hazigandi na rail on ya papa wemba.
We miss you....R.I.P Amina Chifupa.

Geah Habib,mimi,Zamaradi katika super friday...super leo tena.

Dian na kipindi chake chake LEO TENA na 88.4 Redio ya watoto wa mjini
 Nimefanya kazi kwa miaka 4 sasa sijawahi kuchukua likizo,ila safari hii nimeamua kupumzika nikasalimie ndugu jamaa na marafiki.Namuacha Gea Habib atakaimu nafasi yangu na atakupa kitu roho inapenda.Tuombeane heri nikirudi tuendelee kuwa pamoja tena katika leo tena.

 Ml Criss kipindi hicho anafanya Dr.Beat kabla ya kuitwa Xxl...kwa sasa yupo choice fm(102.6 fm) radio nyingine chini ya clouds entertainment...

Filamu mpya ya REY
PRETTY GIRL

baadhi ya wajumbe ya kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Kagera wakiwa katika picha ya pamoja wakati wakisubili kuupokea mwenge ulioanza mbio zake mkoani Kagera wakati ukitokea mkoani Mwanza.Picha na Audax Mutiganzi.

mkuu wa mkoa wa Mwanza, Abbas Kandoro akimkabidhi mwenge wa uhuru mkuu wa mkoa wa Kagera Mohamed Babu

kamanda wa jeshi la polisi mkoani Kagera Henry salewi akipokea mwenge toka kwa mkimbiza mwenge kitaifa Dr. Nassoro Ali Matunzya.

Gari aina ya Subaru lenye namba za usajiri T 193 AZL ikiwa katika hali mbaya sana mara baada ya kupata ajali jioni hii maeneo ya Kinondoni,Ubalozi wa Ufaransa.gari hii ambayo ilikuwa ikitokea maeneo ya Kinondoni Morocco kuelekea mjini,ilipoteza muelekeo mara baada ya gari moja kuingia ghafla katika barabara kubwa huku gari hii ikiwa katika mwendo wa kasi sana na kumfanya dereva wa gari hii kushindwa kuikontroo gari hii na kwenya kugonga moja ya nguzo za taa za barabarani na kuifanya ikapinduka.ndani ya gari hii kulikuwemo na watu watatu ambao wawili walijeruhiwa na kukimbizwa hospital na mwingine kufanikiwa kutoka bila jeraha lolote.




OBAMA akiwa ndani ya White House USA

Rais Barack Obama wa Marekani akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wetu nchini humo Mh. Balozi Mwanaidi Maajar (katikati) pamoja na mume wake, Bw. Shariff Hassan Maajar pamoja na mjukuu wao Kai-Hassan katika Ikulu ya Marekani wakati alipokabidhi hati ya utambulisho.

JK akimnadi MO Jimbo la Singida Mjini.



MO akiwawasalimia wana Singida Mjini mara baada ya kunadiwa na JK katiika mkutano wa kampeni uliofanyika jana Jimboni humo


Wilson Elisha Khambaku akiongea kwa hisia kwenye mkutano wa kampeni Ikungi kuhusu siku 29 alizokaa Chadema baada ya kuanguka kwenye mchakato wa CCM

Wilson Elisha Khambaku akiongea na wana Ikungi katika mkutano wa kampeni.

 
====================
  • Alikaa Chadema siku 29
  • Atoa siri, Chadema hakuna sera
  • Wapinzani zaidi ya 50 warudi CCM
  • Wasanii watoa buradani ya kishindo

Aliyeshindwa kura za maoni jimbo la Singida Magharibi na kuhamia Chadema kwa siku 29, Bwana Wilson Elisha Khambaku, ameeleza kilichomsibu akiwa kwenye chama hicho pinzani.

Akitoa ushuhuda kwenye mikutano ya kampeni Puma na Ikungi, Khambaku alikiri kughafilika na kukimbilia upinzani baada ya kuanguka kwenye kura za maoni.

Akishangiliwa na umati wa watu pale aliposema kwamba aliomba sera za Chadema kwa wiki moja bila mafanikio na hatimaye kushindwa kupata muelekeo wa chama hicho kwa ajili ya kampeni.

Alisema chama hicho ni matapeli kwani baada ya kumzungusha wiki mbili walimpa sera za matusi na kubeza mafanikio thabiti ya CCM.

Akiongelea mafanikio ya CCM kwenye upanuzi wa elimu ambapo hata Umoja wa Mataifa umetambua na kuipa Tanzania tuzo ya kukidhi malengo ya milenia kwenye upande wa elimu kwa asilimia 95.

Akizungumza kwa hisia kubwa, Khambaku alisema siku 29 alizokaa Chadema zilikuwa za mateso na upweke mkubwa, akizifananisha na nyumba yenye kunguni na chawa ambazo humuwasha mtu anayelala kwenye malazi yake.

Amesema sababu kubwa zilizomfanya yeye kurudi CCM ni amani na utulivu iliyodumishwa na CCM tangu uhuru hadi leo. Amewasihi wananchi wa Singida wasifanye makosa ya kuchagua upinzani, ni wasanii, wana chuki na wanabeza hata mafanikio halali ya CCM.

"Mwisho nawasihi msifanye makosa niliyofanya mimi, msihangaike na wapinzani. Hawana sera hao, nimejionea mwenyewe! Naomba mchague chama madhubuti, CCM"

Alimaliza Khambaku huku akishangiliwa na umati mkubwa wa watu.

Na kwenye mkutano wa kampeni wa Ikungi, wapinzani zaidi ya 50 kutoka Chadema na CUF walirudisha kadi zao na kuingia CCM.

Aliyehama kutoka Chadema, alitoa ushuhuda kwa kusema alipochukua kadi ya Chadema aliambiwa kwamba yeye ni mwenyekiti.

"Nikawauliza mwenyekiti wa nini, wakasema wa kijiji hiki. Nikawahoji nani kanichagua? na ninamuongoza nani? Sikupewa jibu, sasa narudi CCM" Alisema Mzee huyo akishangiliwa na umati wa watu.

Nao wasanii wa muziki hawakuwa nyuma kwenye kutoa hamasa kwenye mkutano huo. Mwanamuziki Flora Mbasha akisindikizwa na wanamuziki wengine mashuhuri Ray C na Bushoke walitoa hamasa kubwa kwa wananchi wa Ikungi waliohudhuria kwa wingi mkutano huo wa kampeni.

Naye mshairi maarufu kutokea hapa Singida alitumbuiza kwa shairi lake lililomshukuru Mheshimiwa Kikwete kwa kuleta wilaya mpya ili kusogeza shughuli za maendeleo karibu na wananchi.

Mshairi huyo alisifia umahiri wa Chama Cha Mapinduzi haswa kuwatayarisha viongozi wa nchi na utawala mzima wa chama. Alisema kutoka umoja wa vijana kuna jumuiya ya wazazi na wanawake ambazo zote zinalenga kuwalea wana CCM kuongoza chama na nchi. Alihoji wapinzani wanapikwa namna hiyo hadi kutaka kugombea uongozi wa juu wa nchi?

Akishangiliwa na umati wa watu, mshairi huyo alisihi pia kudumisha amani na mshikamano haswa kipindi cha uchaguzi. Aliwasihi wana Singida kujitokeza kwa wingi kupiga kura ili mkoa uongoze kwenye kura nyingi kwa wagombea wote wa CCM.

Kabla ya Mkutano wa Ikungi - Singida Mashariki, Mheshimiwa Kikwete alifanya mkutano wa kampeni Puma Singida Magharibi ambapo mgombea ubunge wa jimbo hilo Mohamed Missanga alimshukuru Mheshimiwa Kikwete kwa kuwapatia wilaya mpya na jimbo jipya la uchaguzi.

Baada ya hapa, msafara wa Mheshimiwa Kikwete utaelekea Itigi, Manyoni, Kitinku na hatimaye Dodoma Mjini kwa mkutano wa mwisho wa kampeni kwa siku ya leo.

kwa habari hizi na zingine nyingi katika kampeni ya JK

MO akiwahutubia wana Singida Mjini

Wana CCM wakisikiliza mkutano

JK akiwa na MO pamoja na watoto waliokuwepo wakati wa kumpokea alipokuwa akiingia katika hospitali ya rufaa inayojengwa Singida



Wana CCM wakiwa wamelizunguka gari la JK

 
Maalim Seif akimpa kadi mwanachama mpya wa CUF

 
Picha za ufunguzi wa kampeni wa CUF

 

 
                                       Maalim Seif aitangaza ilani ya chama cha wananchi CUF 

 

 

Maalim seif akitoa hutuba baada ya kuchaguliwa kuwa mgombea uraisi wa znz